Jumatatu, Januari 25, 2016

MICHUANO YA CHAN WIKI HII

Michuano ya soka ya mataifa ya Afrika iliendelea kurindima wiki hii; baadhi ya timu zikibanduliwa nje ya mashindano hayo ya kieneo huku zingine zikifanikiwa kusonga mbele. Timu ya Kodivaa imezidi kupata mafanikio katika kipute hicho na sasa imetinga robo fainali ya michuano hiyo baada ya kuibamiza Gabon mabao 4-1 siku ya Jumapili. Mali imepata ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Zimbabwe katika kundi D, mchuano ambao ulipigwa mjini Rubavu. Goli hilo la dakika ya 82 lilitiwa kimyani na mshambuliaji Moussa Sissoko.
Kwa ushindi huo Mali sasa inaongoza kundi hilo ikiwa na alama 4 kabla ya kutoana kijasho na Uganda yenye alama 1 na Zambia yenye alama 3. Wakati huo huo Zambia imekata tiketi yake ya robo fainali kwa kuishinda Uganda 1-0 mjini Rubavu. Goli hilo la vijana wa Chipolopolo lilifungwa na mwanasoka wa muda mrefu Christopher Katongo kunako dakika ya 41 ya mchezo. Kwa kichapo hicho Uganda imejiweka katika katika mazingira magumu ya kutinga hatua ya mchujo. Uganda italazimika kushinda mechi yake ya mwisho dhidi ya Zimbabwe na kutegemea Zambia kuishinda Mali ilhali Mali itahitaji tu matokeo ya sare. Morocco, ambayo imefungwa na Rwanda mabao 4-1, pamoja na Gabon ambazo zote ni za kundi A, zimeaga michuano hiyo ya CHAN 2016. Morocco inachukua nafasi ya 3, nayo Gabon inachukua nafasi ya 4. Mpaka sasa Rwanda ndio ipo kileleni mwaa kundi A huku Kodivaa ikiwa katika nafasi ya pili katika kundi hili.

0 comments:

Chapisha Maoni