Jumatatu, Januari 25, 2016

MICHUANO YA KOMBE LA PREMIER

Licha ya kuwa ugenini, lakini mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya soka ya Uingereza klabu ya Chelsea imepata ushindi muhimu sana msimu huu ingawaje ulikuwa wa bao 1-0 dhidi ya wabeba bunduki wa London vijana wa Arsenal. Hata hivyo huenda Arsenal walilambishwa chini kwa kuchapwa bao moja la uchungu, kwa kuwa walilazimika kusakata kabumbu hiyo ya Jumapili wakiwa na nakisi ya mchezaji mmoja, baada ya mlinzi wao Per Mertesacker, kulimwa  kadi nyekundu kwa kumchezea visivyo mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa. Upungufu huo ulimfanya kocha Arsene Wenger kumtoa mshambuliaji mahiri Oliver Giroud na kumwingiza mlinzi Gabriel Paulista. Bao ya Chelsea lilifungwa na kiungo huyo Diego Coasta.
Hata hivyo kocha wa The Blues Guud Hiddinks anahisi kupawa kadi nyekundu kiungo huyo wa Gunners kulistahili na ilikuwa ni hatua ya mantiki.
Kwa kichapo hicho Arsenal wamedondoka hadi katika nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi, wakiwa na alama 44. Man City ambayo ililazimishwa sare ya mabao 2-2 na West Ham ipo katika nafasi ya pili ikiwa na pointi 44 nyuma ya vinara wa ligi kwa sasa Leicester City ambayo ina alama 47 haswa baada ya kuifanyia mauaji ya Stoke City kwa kuicharaza mabao 3-0. Man U pia kama vile Arsenal, walikabiliwa na wakati mgumu pale walipocheza na Southamptom wikendi hii. Mtoka benchi Charlie Austin alifanikiwa kucheka na nyavu za Mashetani Wekundu dakika saba baada ya kuingia uwanjani na kuifanya iridhike na nafasi ya 5 ikiwa na pointi 37. Katikia matokeo mengine ya Ligi ya Premier Ligi wikendi hii, Liverpool iliilaza Norwhich mabao 5-4 wakati ambapo Aston Villa na Westbrom walikuwa wakilazimishana sare ya 0-0. Mchuano wa Sunderland na Bournmouth uliishia kwa sare ya bao 1-1 wakati ambapo Everton ilikuwa ikipokea kichapo cha mabao 2-1 kutoka Swansea.

0 comments:

Chapisha Maoni