Ijumaa, Januari 22, 2016

KAMANDA MKUU WA ALSHABAAB AUAWA

Kamanda mkuu wa kundi la wanamgambo la Alshabab, Maalim Janow, auawa baada ya kupata shambulio la anga kutoka kwa wanajeshi wa Kenya, Mkuu wa majeshi nchini Kenya Jenerali Samson Mwathethe aliuambia mkutano wa wanahabari mjini Nairobi.
akirejelea mauaji ya wanajeshi wa Kenya nchini Somali na wanamgambo wa Alshabab, Jenerali huyo alisema kuwa bomu lililotumika na wapiganaji hao ni mara tatu kwa ukubwa wa lile lililotumika katika ubalozi wa Marekani jijini nairobi mwaka 1998 ambalo liliangusha jumba la ghorofa 10 na kuua zaidi ya watu 200 na kujeruhi wengine 5000.

0 comments:

Chapisha Maoni