Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amekuwa rais wa kwanza aliye madarakani
kufika mbele ya mahakama ya Kimataifa ya ICC. Bwana Kenyatta anakanusha
mashtaka ya uhalifu dhidi ya ubinaadam kuhusiana na madai ya kuhusika
kwake katika ghasia za baada ya uchaguzi miaka saba iliyopita. Sababu ya
shauri mahakamani siku ya Jumatano, ni kutazama iwapo kesi hiyo
iendelee au itupiliwe mbali. Upande wa mashtaka umetaka kesi hiyo
iahirishe kwa muda usiojulikana mpaka pale serrikali ya Kenya
itakapowasilisha kile inachosema nyaraka muhimu. Upande wa utetezi
unasema Bwana Kenyatta hana sababu ya kupanda kizimbani kwa sababu
upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha kesi yake. Uamuzi kamili
unatarajiwa kutolewa baadaye siku zijazo. Picha- Uhuru akiwa mahakamani
AP.




0 comments:
Chapisha Maoni