Mwendesha pikipiki mmoja aliyefahamika kwa jina la Shukurani
Mtafya (20) mkazi wa Nzovwe aliyekuwa akiendesha pikipiki yenye namba za usajili
T.805 BDQ aina ya T-Better amefariki dunia baada ya pikipiki hiyo kuacha njia
na kuanguka.
Ajali hiyo imetokea mnamo tarehe jana majira ya saa 06:00
asubuhi maeneo ya Stand Kuu, kata na tarafa ya Sisimba, jiji na mkoa wa Mbeya.
Chanzo cha ajali kinachunguzwa. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali
ya Rufaa Mbeya kwa ajili ya uchunguzi wa kitabibu.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya kamishina msaidizi
mwandamizi wa polisi Ahmed Msangi anatoa wito kwa madereva na watumiaji wengine
wa vyombo vya moto kuwa makini, kuzingatia sheria na alama za usalama
barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.
0 comments:
Chapisha Maoni