Danguro hatari linaloendesha shughuli zake katika eneo la shule limefichuliwa baada ya
kumnasa mwanamke aliyedai ni mke wa mtu akifanya uzinzi na mtu ambaye hakufahamika mara moja
ambaye hakujulikana jina lakejapokuwa inahisiwa kuwa ni mume wa mtu.
Tukio hilo la aibu ya karne lilijiri ndani ya eneo la shule ya msingi
Shekilango, iliyopo Mapambano, Sinza jijini Dar, hivi karibuni ambapo
mke huyo wa mtu alikuwa akichepuka.
Wawili hao, baada ya kukamatwa wakifanya ngono hadharani walitiwa kizuizini kabla ya
vijana wanaodaiwa kuchukua posho kwa wanaofanyia mambo yao kwenye
danguro hilo kuanzisha vurumai ingawa walidhibitiwa huku jamaa aliyekuwa
anahudumiwa akitoka nduki.
Akizungumza na Fichuo Tz, mwanamke huyo aliomba asamehewe na kusema
kwamba kinachomsababishia kufanya shughuli hiyo ni ugumu wa maisha na
kundi la watoto anaowalea ambao baba yao hana ajira.
Baada ya mtandao huu kutaka kuzungumza na mumewe ili kujua kama anafahamu
kuwa mkewe anafanya biashara haramu ya kuuza mwili, mwanamke huyo alidai
kwamba mumewe hana simu.
Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo alisikika akisema:
Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo alisikika akisema:
Dah! Mngewahi dakika kumi tu, mngemkuta baba wa Kiarabu aliyeingia na mwanamke muda si mrefu, hili danguro linatumiwa usiku kucha, yaani linapoingia giza tu hapa ni balaa hadi asubuhi.
Mwalimu wa zamu, Kilavo Charles, amesema kuwa suala hilo
limeshafikishwa kituo cha Polisi Mabatini ambao waliahidi
kulishughulikia.
Ni aibu, asubuhi watoto wanafagia kondom, tunakosa cha kuwaambia, hii ni hatari kwa kweli na tunaomba mamlaka zinazohusika zilifanyie kazi jambo hili
lisema.



0 comments:
Chapisha Maoni