Jumatano, Oktoba 15, 2014

MATUKIO MAKUBWA KUTOKA MKOANI IRINGA

Watu wawili wanashikiliwa na jeshi la polisi Mkoani Iringa Katika  Matukio mawili tofauti likiwepo la mtu mmoja kushikiliwa kwa tuhuma ya kukutwa akimiliki silaha kinyume cha sheria. Akithibitisha kutokea kwa matukio hayo Kamanda wa jeshi la polisi Mkoani Iringa ACP Ramadhani Mungi amesema askari wanyamapori wakiwa doria wamemkamata John Mapunda mkazi wa kijiji cha Mbwileli wilaya ya Iringa Vijijini Mkoa wa Iringa akiwa na bunduki aina ya SHORTGUN yenye no:66721 akiwa anamiliki bila kibali. Kamanda Mungi ameongeza kuwa baada ya uchunguzi wa kina kufanyika nyumbani kwa mtuhumiwa askari hao walimkuta akiwa na nyama ya swara yenye uzito wa  kilo nne akiwa amezipata kinyume cha sheria. Adha amesema askari polisi wakiwa doria wamekamata Rahedy Joseph umri miaka 23 mkazi wa maeneo ya Ipogoro Manispaa na Mkoa wa Iringa akiwa na madawa ya kulevya aina ya bhangi kete 43 ambazo alikuwa amezihifahi ndani ya hotpoti la chakula,mtuhumiwa ni muuzaji wa madawa hayo. Wakati huo huo amesema askari polisi wanaendelea na msako wa kuwatafuta watu waliohusika tukio la kuvamia kwa nguvu na kufanya ung’anganyi dukani kwa Heppy Ingasi umri miaka 36 mkazi wa maeneo ya Nduli Manispaa na Mkoa wa Iringa. Hata hivyo Kamanda Mungi amesema vitu vilivyoporwa ni simu moja aina ya tecno,fedha taslimu zaidi ya shilingi milioni mbili pamoja na vocha za aina mbalimbali zenye thamani ya shilingi milioni tatu na nusu ambapo watuhumiwa hao walitumia panga kumshambulia mwenye duka.

0 comments:

Chapisha Maoni