Jumatatu, Septemba 29, 2014

TAREHE YA LEO KATIKA HISTORIA

Siku kama ya leo miaka 22 iliyopita, ulifanyika uchaguzi huru wa kwanza nchini Angola. Katika uchaguzi huo chama cha MPLA kilichokuwa kikiongoza nchini humo tangu mwaka 1976 kilipata ushindi na kiongozi wake Jose Edward Dos Santos akachaguliwa tena kuingoza nchi hiyo. Ni vyema kuashiria hapa kwamba, Angola ilitumbukia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe baada ya kupata uhuru kutoka kwa mkoloni Mreno hapo mwaka 1975. Vita vya ndani nchini humo vilihitimishwa rasmi mwaka 2002 baada ya kuuawa kiongozi wa chama cha upinzani cha UNITA Jonas Savimbi.
Siku kama ya leo miaka 33 iliyopita, muwafaka na tarehe 7 Mehr 1360 Hijria Shamsia, aliuawa shahidi Hujjatul Islam Sayyid Abdul Karim Hasheminejad mwanachuoni na mwanamapambano shupavu wa Iran katika mji wa Mashhad. Sayyid Hasheminejad aliuawa shahidi baada ya kupigwa risasi na mmoja wa wanachama wa kundi la Munafikiin. Mwanachuoni huyo alikuwa mstari wa mbele katika harakati za mapinduzi nchini Iran dhidi ya utawala wa Shah, na aliwahi kuteswa na kuwekwa gerezani mara kadhaa.
Siku kama ya leo miaka 113 iliyopita, alizaliwa mwanafizikia mashuhuri wa Italia Enrico Fermi katika mji wa Roma. Baada ya kukamilisha masomo ya chuo kikuu aliweza kuvumbua kanuni ya Mwendo wa Molekuli ya Gesi. Fermi alifanya uchunguzi kuhusu mabadiliko ya atomu na akafanikiwa kutengeneza betri ya atomu kwa kuipasua na kutoa nje nishati yake. Mwanafizikia huyo wa Italia alifariki dunia mwaka 1954.
Na miaka 96 iliyopita muwafa na leo, nchi ya Bulgaria ilisalimu amri baada ya kushindwa mara kadhaa katika Vita Vikuu vya Kwanza vya Dunia. Bulgaria ilikuwa pamoja na Ujerumani, utawala wa Othmania, Austria na Hungary na zilikuwa zikipigana dhidi ya Ufaransa, Russia, Uingereza na Italia. Baada ya Bulgaria kushindwa katika vita vya Macedonia, Desemba 15 mwaka 1918 ilitia saini Mkataba wa Salonica katika mji wenye jina hilo nchini Ugiriki ya leo.

0 comments:

Chapisha Maoni