Alhamisi, Septemba 25, 2014

RAIS GOODLUCK JONATHAN: BADO TUNAWATAFUTA WATOTO WALIOTEKWA NA BOKO HARAM

Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria amesema katika Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwamba, maafisa wa nchi yake bado wanafanya jitihada za kuwakomboa wasichana wa shule karibu 200 waliotekwa nyara na kundi la kigaidi la Boko Haram mwezi Aprili. 
Rais Jonathan ameongeza kuwa, ingawa miezi zaidi ya mitatu imepita tangu wasichana hao wa shule watekwe nyara, lakini hawajaacha kufanya jitihada za kuwakomboa. Rais wa Nigeria anakosolewa ndani na nje ya nchi kwa kuchelewa kuchukua hatua za kuwakomboa wasichana hao waliotekewa nyara na Boko Haram na kushindwa kulitokomeza kundi  hilo.
Wakati huo huo, jeshi la Nigeria limetangaza kwamba, zaidi ya wapiganaji 135 wa kundi la Boko Haram wamejisalimisha kwa vikosi vya usalama vya serikali na kukabidhi silaha zao huko kaskazini mashariki mwa nchi. 

0 comments:

Chapisha Maoni