Alhamisi, Septemba 25, 2014

MTOTO AGONGWA NA GARI NA KUFARIKI IRINGA

Mtu mmoja amefariki mkoani Iringa baada ya kugongwa na gari. Akithibitisha kutokea kwa matukio hayo kamanda wa jeshi la polisi Mkoani Iringa ACP Ramadhani Mungi amesema Kelsensia Bonifasi umri miaka 7 mwanafunzi wa dalasa la kwanza shule ya msingi Sun Academy iliyopo maeneo ya Isakalilo Manispaa na mkoa wa Iringa amefariki papo hapo baada ya kugongwa na gari lenye namba za usajili T.306 CRM aina ya toyota Hiace.
Kamanda Mungi ameongeza kuwa ajali hiyo imetokea katika barabara ya Iringa-Kalenga Manispaa na Mkoa wa Iringa, chanzo kikiwa ni mwendo kasi na dereva wa gari hilo Rajabu Adamu umri miaka 28 mkazi wa eneo la Kihesa Manaispaa ya Iringa anashikiliwa na jeshi la polisi kwa uchunguzi zaidi.

0 comments:

Chapisha Maoni