Alhamisi, Septemba 25, 2014

JAMAA AMBAKA MTOTO WA MIAKA 12 IRINGA

Maneno Ilave mwenye umri wa miaka 21 mkazi wa maeneo ya Mkwawa Manispaa na Mkoa wa Iringa anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kumbaka na kumsababishia maumivu makali ya mwili mtoto mwenye umri wa miaka 12.
Hata hivyo Kamanda wa jeshi la Polisi mkoani Iringa ACP Ramadhani Mungi amesema chanzo cha tukio hilo ni tamaa ya mapenzi pia ametoa wito kwa walezi na wazazi kuwa makini katika malezi ya watoto wao ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanacheza sehemu za wazi na kuwahi kurudi nyumbani.

0 comments:

Chapisha Maoni