Ijumaa, Septemba 19, 2014

GRANIT XHAKA AOKOTA SIMU UWANJANI KATIKA MECHI

Usiku wa kuamkia hii leo ulikuwa maalum katika historia ya kuanza tena kwa michuano ya ligi ya barani Ulaya *Europa League* msimu huu katika hatua ya makundi, ambapo klabu kadhaa za mataifa mbali mbali barani humo zilipambana kwa lengo la kusaka point tatu muhimu.
Nchini Ujerumani wakati historia hiyo ikiandikwa, wenyeji Borussia Monchengladbach walikuwa wakipambana na klabu Villarreal kutoka nchini Hispania huko Stadion im Borussia-Park.
Katika mchezo huo ambao ulimalizika kwa sare ya bao moja kwa moja, kiungo wa Borussia Monchengladbach, Granit Xhaka aliustaajisha ulimwengu wa wapenda kandanda baada ya kukota simu katika sehemu ya kuchezea.
Kitendo cha mchezaji huyo kuokota simu uwanjani kilifanyika wakati mpambano ukiendelea, hatua ambayo iliwalazimu wapiga picha kufuatilia kwa ukaribu kwa kutaka kubaini ni nini kilichookotwa na Granit Xhaka.
Hata hivyo baada ya kuiokota simu hiyo, Granit Xhaka alipeleka moja kwam moja kwa muamuzi wa mchezo huo, kwa ajili ya kupisha mambo mengine yanayohusu mpambano huo kuendelea.
Lakini baada ya mchezo huo kumalizika mmoja wa maafisa wa benchi la ufundi la klabu ya Monchengladbach, alidai simu hiyo ilikuwa ya kwake lakini haikufahamika ni wakati gani aliiangusha uwanjani ama ilifika vipi katika sehemu ya kuchezea.

0 comments:

Chapisha Maoni