Siku kama ya leo miaka 45 iliyopita, sawa na Agosti 21 mwaka 1969,
Masjidul Aqsa kibla cha kwanza cha Waislamu, kilichomwa moto na
Wazayuni. Katika tukio hilo, eneo hilo takatifu na la kihistoria
liliharibiwa vibaya sana. Utawala wa Kizayuni wa Israel ulidai kuwa,
kitendo hicho kilifanywa na mtalii wa Kiaustralia. Utawala huo wa
Kizayuni ulitayarisha mahakama ya kimaonyesho tu mjini Tel Aviv, na
kuchukua uamuzi wa kumuachilia huru mtuhumiwa huyo kwa madai kwamba
alikuwa na matatizo ya kiakili. Baada ya kutokea kitendo hicho, nchi za
Kiislamu zilikutana na kuamua kuunda Jumuiya ya Nchi za Kiislamu (OIC)
ili kukabiliana na hatari zinazoukabili ulimwengu wa Kiislamu na
matukufu yake.
Tarehe 21 Agosti miaka 55 iliyopita, iliasisiwa The Central Treaty
Organization ambayo ilikuwa ikijulikana kwa jina la Cento na kuchukua
nafasi ya mkataba wa Baghdad. Taasisi hiyo iliundwa na Iran, Uturuki,
Pakistan na Uingereza mjini Ankara, Uturuki. Japokuwa Marekani haikuwa
mwanachama rasmi wa Taasisi ya Cento na ilishiriki kwenye vikao vya
jumuiya hiyo kama mtazamaji tu, lakini ilikuwa na nafasi kuu katika
maamuzi yote ya taasisi hiyo. The Central Treaty Organization ilivunjika
baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran na kujiondoa nchi
hiyo katika mkataba huo mwaka 1979.
0 comments:
Chapisha Maoni