Mapigano makali yameshuhudiwa kati ya jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia
ya Congo na wanamgambo wa Mai-Mai katika maeneo ya mashariki mwa nchi
hiyo. Taarifa zinasema kuwa, mapigano hayo yalitokea katika eneo moja
kaskazini mwa mkoa wa Kivu Kaskazini. Duru za jeshi la Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Congo zimetangaza kuwa, mapigano hayo yalijiri kati ya
jeshi la nchi hiyo na wanamgambo wa Mai-Mai Cheka. Taarifa zaidi
zinasema kuwa, jeshi la Congo limefanikiwa kuwafurusha wanamgambo hao
kutoka katika maeneo hayo. Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
limefanikiwa katika mapigano hayo kuangamiza silaha za wanamgambo hao na
kwamba, sasa jeshi hilo linayadhibiti maeneo hayo.
Hayo yanajiri katika hali ambayo, hivi karibuni Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilieleza wasiwasi wake juu ya kuongezeka machafuko katika maeneo ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Maeneo ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo yamekuwa yakikabiliwa na machafuko ya mara kwa mara kutokana na kuweko harakati za makundi ya waasi.
Hayo yanajiri katika hali ambayo, hivi karibuni Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilieleza wasiwasi wake juu ya kuongezeka machafuko katika maeneo ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Maeneo ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo yamekuwa yakikabiliwa na machafuko ya mara kwa mara kutokana na kuweko harakati za makundi ya waasi.




0 comments:
Chapisha Maoni