Jumanne, Julai 29, 2014

UMUHIMU WA MAZOEZI ILI KUONGEZA UREMBO

Mazoezi ni muhimu kwa mwanadamu kwa ajili ya kuuweka mwili katika hali nzuri kiafya, lakini wengi wetu tumekuwa wavivu sana kufanya mazoezi hata ya kutembea. Kwa upande wa wanawake wa hapa nchini hili ni tatizo kubwa. Wanawake wengi hapa nchini ni wavivu katika kufanya mazoezi na ndio sababu wengi wana vitambi na hivyo watu wengi kudhani kwamba wana ujauzito. Urembo kwa mwanamke unajumuishwa na muonekanao wa mwili kama umekaa katika shepu nzuri. Sura siyo hoja sana, bali maumbile. kuna baadhi ya wanawake wamejaaliwa kuwa na sura na maumbo mazuri lakini baada ya kufakamia bia na nyama choma hususan kiti moto huumuka na kuwa na maumbo makubwa na mabaya yasiyo na mvuto.
Mazoezi hayahitaji gharama, maana wengi hapa watakuja kulalamika kwamba hawana fedha za kwenda Gym.

0 comments:

Chapisha Maoni