Taarifa za kuwepo beef kati ya wasanii wakubwa wa Nigeria Wizkid na
Davido wakitambiana nani anafunika zaidi zinaendelea kukorezwa na tweets
za vijembe kati yao kila kukicha.
Ingawa wawili hao waliwahi kuonekana katika picha ya pamoja na kutoa
ishara ya kumaliza tofauti zao, bado maandishi yao yanaonekana kuwa
mwiba kwa kila mmoja.
Mkali wa Kukere ameamua kutoa ushauri wake kwa wasanii wa Nigeria,
ushauri ambao unaonekana kumwagusa moja kwa moja Wizkid na Davido ingawa
hakuwataja majina.
“Acheni kuongea!!! Tuachie muziki zaidi!!! Tuwaburudishe mashabiki!!! Acheni chuki!!! Maombi yangu ni kwamba wote tufanikishe.”
0 comments:
Chapisha Maoni