Nchini
Marekani, baraza la wawakilishi ambalo linadhibitiwa na chama
cha Republican limepiga kura kuwasilisha mahakamani kesi dhidi
ya rais Barack Obama. Hatua hiyo inawaruhusu wanasheria wa bunge
hilo kuandika waraka wa sheria unaotarajiwa kudai kuwa Obama
alikiuka mamlaka yake wakati alipofanya mabadiliko katika sheria
ya matumizi ya afya, yanayofahamika kama "Obamacare". Obama
anadai kuwa alitumia madaraka yake kama hatua ya mwisho baada
ya bunge la Marekani kukataa kushirikiana naye kufanya kazi.
0 comments:
Chapisha Maoni