Ijumaa, Juni 13, 2014

TETESI ZA USAJILI KATIKA MAGAZETI YA ULAYA LEO

Mshambuliaji wa Chelsea Romelu Lukaku amekataa kwenda West Ham kwa mwaka wa pili sasa, lakini huenda akajiunga na Wolfsburg ya Ujerumani (Daily Mirror), Manchester United sasa wamemgeukia kiungo wa Bayern Munich, Bastian Schweinsteiger baada ya kushindwa kumpata Thomas Muller (Daily Star), Arsenal wapo tayari kutoa pauni milioni 5 kwa kipa Pepe Reina (Metro), Arsenal pia wanataka kumsajili beki Bressan kutoka Gremio ya Brazil (Daily Express), Arsene Wenger pia anakaribia kukamilisha usajili wa Carlos Vela kutoka Real Sociedad (Sun), Liverpool wana imani wataweza kumsajili Max Meyer kutoka Schalke na kuwapiku Arsenal na Chelsea (Daily Express), kiungo wa Barcelona, Alex Song ameambiwa yuko huru kuondoka Nou Camp, huku Manchester United wakimfuatilia mchezaji huyo wa zamani wa Arsenal (Talksport), rais wa Real Madrid Florentino Perez ameruhusu klabu yake kumfuatilia Ramires wa Chelsea (Marca), Paris St-Germain itamfuatilia kipa Petr Cech iwapo Chelsea hawatamhitaji (Le Figaro), Atlètico Madrid wanafikiria kutoa pauni milioni 18 kumsajili kiungo wa Arsenal Santi Cazorla (As.com).

0 comments:

Chapisha Maoni