Jumanne, Juni 10, 2014

RAIS SALVA KIIR NA MUASI RIEK MACHAR KUKUTANA LEO

Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini leo atakutana na kufanya mazungumzo na Riek Machar, kiongozi wa wanamgambo waasi nchini humo huko Addis Ababa, Ethiopia, ikiwa ni katika juhudi za kukomesha vita vilivyodumu kwa miezi sita nchini humo.
Inatarajiwa kuwa, viongozi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Kieneo ya Mashariki mwa Afrika IGAD watashiriki kwenye mazungumzo hayo. Hii ni mara ya kwanza kwa viongozi hao hasimu kukutana tokea yalipotiwa saini makubaliano ya kusimamisha vita yaliyofikiwa tarehe 9 mwezi uliopita. Mgogoro wa nchi hiyo uliingia kwenye hatua mpya baada ya pande hizo mbili kukiuka mara kwa mara makubaliano ya usitishaji vita.
Kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Mataifa, hadi sasa maelfu ya watu wameuawa na zaidi ya watu milioni moja na laki tatu wamelazimika kuwa wakimbizi ndani na nje ya Sudan Kusini.

0 comments:

Chapisha Maoni