ZAIDI ya wagonjwa 40 waliolazwa katika wodi ya Sewa Haji katika
Hospitali ya Taifa Muhimbili, wanalala chini kwenye magodoro kutokana
na ukosefu wa vitanda.
Hali hiyo imebainika baada ya wananchi na wagonjwa waliolazwa wodini
hapo kutoa malalamiko yao na Tanzania Daima kushuhudia hali hiyo.
Tanzania Daima ilipofika wodini hapo, iliona wagonjwa hao wakiwa
wamelala chini, huku wengine wakiwa wamelala kwenye korido kutokana na
mlundikano wa wagonjwa.
Hatuelewi Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii bungeni anadai bajeti ya nini wakati Hospitali ya Taifa inatia aibu, haina vitanda wala vyandarua
alisema mmoja wa wananchi waliofika wodini hapo kuona
wagonjwa wao.
Juhudi za kumtafuta msemaji wa hosptali hiyo kuzungumzia tatizo hilo,
ziligonga mwamba baada ya kutokuwepo ofisini kwake na simu yake ya
kiganjani kutopatikana.
Wakati huohuo, mlinzi wa wodi hiyo alijikuta katika wakati mgumu
baada ya kuwazuia watu waliofika hospitalini kuingia na maji na matunda
na kudai muda huo (saa 6:30 mchana) ni wa chakula pekee, na kwamba
muda wa kuleta matunda, juisi na maji ni saa 10 jioni.
Kutokana na hali hiyo, watu hao walianza kufanya vurugu na kuingia
kuwaona wagonjwa wao huku wakidai kuna baadhi ya wagonjwa hawali
chakula wanatumia juice na matunda.
0 comments:
Chapisha Maoni