Jumanne, Juni 03, 2014

MTOTO MCHANGA AUAWA KWA KUFUNGWA BANDEJI MDOMONI NA PUANI

KATIKA hali isiyo ya kawaida mwanamke mmoja ambaye hakujulikana jina lake wala kujua anapoishi, anasadikika kutenda ukatili na unyama wa hali juu kwa kumuua mwanaye na kisha kumtupa pembezoni mwa barabara ya kwenda Kawe-Beach.
Wavuvi wa eneo hilo waliona mfuko pembezoni ukiwa na damu hali ambayo iliwashtua na kuamua kusogea karibu ndipo walipomkuta mtoto huyo mwenye jinsi ya kike akiwa amefariki huku akiwa amefungwa plasta mdomoni na puani.

0 comments:

Chapisha Maoni