Jumamosi, Juni 07, 2014

MAXIMO KULA MILIONI 19 KWA KILA KOMBE YANGA

WAKATI ujio wa Kocha Marcio Maximo ukiwa njiani kukamilika, ambapo mpaka sasa ni asilimia 95, klabu ya Yanga ipo tayari kumpa mamilioni kila atakapofanikiwa kubeba taji.
Habari za uhakika kutoka ndani ya Yanga zinaeleza kuwa pamoja na gari la kutumia na nyumba ya kuishi, Mbrazili huyo amepewa ofa ya dola 12,000 (Sh milioni 19) kila atakapobeba ubingwa wa Tanzania Bara au Kombe la Cecafa.
Imeelezwa kuwa katika mazungumzo yanayoendelea kati ya Yanga na Maximo suala hilo limeshapitishwa moja kwa moja, na pia kuna ofa nyingine iliyozungumzwa kuwa iwapo ataifikisha Yanga katika hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho, pia atapewa kitita cha kama hicho cha dola 12,000.
Mmoja wa watu wa karibu na wakala anayeshughulikia suala la Maximo kuja nchini ameliambia Championi Jumamosi kuwa mambo yanakwenda vizuri na Maximo amevutiwa na ofa hizo.

0 comments:

Chapisha Maoni