Alhamisi, Juni 12, 2014

KYELA YATEKETEZA POMBE HARAMU VIROBA

Mamlaka ya Chakula na Dawa kwa kushirikiana na uongozi wa wilaya za Rungwe na kyela wamefanikiwa kukamata na kuteketeza shehena kubwa ya pombe haramu aina ya viroba, vipodozi, dawa na vyakula ambavyo muda  wake wa matumizi umepita, bidhaa ambazo zimekamatwa wakati wa operesheni ya kutokomeza uingizwaji wa pombe haramu za viroba mkoani mbeya.
Shehena ya pombe haramu za viroba, vipodozi, vyakula na dawa ambazo muda wake wa matumizi umekwisha vikiwa na thamani ya zaidi ya shilingi milioni 20 vimeteketezwa kwa nyakati tofauti katika wilaya za rungwe na kyela, zoezi ambalo limesimamiwa na kamati za ulinzi na usalama za wilaya hizo.
Mkuu wa idara ya usafi na mazingira wilayani rungwe Dk. Nimroud kipoza na afisa wa mamlaka ya mapato TRA wilayani kyela Paul Walalaze wanaelezea madhara ya bishaa hizo kiafya na kiuchumi kwa watanzania. 
Baadhi ya vijana ambao wameunda kikundi cha kupambana na pombe haramu za viroba pamoja na dawa za kulevya katika mpaka wa kasumulu wilayani kyela wamesema mafanikio yao katika kudhibiti bidhaa hizo yanatokana na kupata ushirikiano mzuri kutoka serikalini.
Meneja wa mamlaka ya udhibiti wa chakula na dawa (TFDA) kanda ya nyanda za juu kusini, Rodney Alananga amesema zoezi la kupambana na bidhaa hizo ni endelevu, hivyo akawataka wale wote wanaojihusisha na biashara hiyo kuacha ili kuepuka kupata hasara.

0 comments:

Chapisha Maoni