Alhamisi, Juni 12, 2014

KOMBE LA DUNIA KUTIMUA VUMBI KUANZIA LEO BRAZIL

Macho ya walimwengu na wapenzi wa soko dunia hii leo yanaelekezwa nchini Brazil ambako masaa machache yamesalia hadi kuanza mashindano ya Kombe la Dunia katika mchezo wa soka.
Mechi ya ufunguzi wa mashindano hayo  yanayozikutanisha timu za  mpira wa miguu kutoka nchi 32 duniani, itatanguliwa na hafla za ufunguzi zitakazofanyika katika mji wa Sao Paul  ambazo zinaenzi mazingira, watu na mpira wa miguu.
Serikali ya Brazil inatumia jeshi la anga, askari polisi na wanajeshi 147,000 kuimarisha usalama huku shule za nchi hiyo zikifungwa wakati huu wa mashindano hayo. Mechi ya ufunguzi wa mashindano ya Kombe la Dunia katika mchezo wa soka itafanyika katika uwanja wa Itaquerao kati ya mwenyeji Brazil na Croatia.
Hayo yanajiri huku kukishuhudiwa migomo na malalamiko ya wananchi ambapo Rais Dilma Rousseff wa Brazil ametetea uamuzi wa serikali yake wa kuwa mwenyeji wa mashindano hayo, na kutupilia mbali madai kwamba wametumia gharama kubwa kuanda mashindano hayo. Ametangaza kuwa matayarisho yamekamilika na kusisitiza kuwa uwekezaji katika ujenzi wa viwanja vya mpira, viwanja vya ndege na miundombinu mingine utaipa nchi hiyo faida za muda mrefu.  Rais wa Brazil pia amewataka wananchi wa nchi hiyo ya Amerika ya Latin kuunga mkono timu ya taifa hilo na kuwakirimu wageni na watalii.

0 comments:

Chapisha Maoni