Ijumaa, Juni 13, 2014

FIFA 2014 BRAZIL: MEXICO1-0CAMEROON

Mexico yajikita katika nafasi ya pili ya Kundi A nyuma ya Brazil baada ya ushindi wa bao moja kwa nunge dhidi ya wawakilishi wa Afrika the Indomitable lions ya Cameroon.
Mechi hiyo ndiyo iliyokuwa ya pili baada ya ushindi tata wa Brazil dhidi ya Craotia hapo jana.
Kama mechi hiyo ya ufunguzi iliyoshuhudia maamuzi tata, Mabao mawili ya mshambulizi wa Giovanni Dos Santos yalifutiliwa mbali kutokana na kile wachambuzi wa mechi waliashiria kuwa ni makosa ya naibu wa refarii.
Licha ya hayo Mkwaju wa Dos Santos ulipanguliwa na kipa wa Cameroon kabla ya Oribe Peralta kufuma bao hilo la pekee na la ushindi kunako dakika ya 61 ya kipindi cha pili.
Mexico sasa inatoshana nguvu na Brazil kileleni mwa kundi A.
20:55 Mechi imekamilika Mexico 1-0 Cameroon
20:53 Hernandes anapoteza nafasi ya wazi ya kuongeza bao la pili la Mexico.
20:53 Dakika nne za ziada Mexico 1-0 Cameroon
Mexico 1-0 Cameroon
20:51 Mexico 1-0 Cameroon Dakika ya 90 .
20:44 Matokeo bado ni Mexico 1-0 Cameroon dakika ni ya 82
20:42 Mexico wanashambulia lango la Cameroon zikiwa zimesalia dakika 8 tu ya mechi hii ya Kundi A
20:41 Mkwaju unapigwa na kupanguliwa mara moja na Mexico,inakuwa Goal Kick.
20:41 Samuel Etooooo ah ! ,,,Kona kuelekea lango la Mexico.
20:40 Badiliko la Cameroon A. Song aondoka na nafasi yake inatwaliwa na WeBo.
20:39 Matokeo bado ni Mexico 1-0 Cameroon dakika ni ya 78
20:38 Free Kick kuelekea lango la Cameroon
20:35 Kufikia sasa Mexico wametawala mechi hii kwa asilimia 65 % huku Cameroon wakicheza asilimia 35 %
20:32 Javier Hernandez anachukua nafasi ya mfungaji bao la Mexico Oribe Peralta
20:31 Mabao bado ni Mexico 1-0 Cameroon Kunako dakika ya 70 ya kipindi cha pili
Peralta Oribe Mfungaji bao la pekee la Mexico.
20:31 Dakika ni ya 69 ya kipindi cha pili.
20:29 Mexico wafanya badiliko la kwanza Andres naondoka Marco anachukua nafasi yake uwanjani .
20:21 BAOOOOOO Mexico 1-0 Cameroon
20:20 Na sasa Mexico wanajibu Mashambulizi 'First Break ya Mexico.
20:19 Mkwaju wa Freekick unagonga ukuta na sasa ni Kona.
20:17 Hector Moreno anaoneshwa kadi ya njano kwa kumwangusha Etoo.
20:16 Uwanja umelowa maji lakini Samuel Ettoo anajaribu kukwepa safu ya ulinzi ya Mexico.
20:16 Mabao bado ni Mexico 0-0 Cameroon
20:15 Tupe maoni yako kwenye facebook tafuta BBCSwahili na utuwachie ujumbe wako.
20:15 Je mabao ya Giovani yaliyokataliwa yalikuwa halali ?
20:13 Cameroon wafanya shambulizi lao la kwanza katika kipindi cha pili katika lango la Mexico lakini mkwaju ni hafifu mno .
20:11 Dos Santos bado amelala chini refarii anapeana mkwaju wa adhabu.
20:10 Dos Santos ni mwiba katika safu ya ulinzi ya the Indomitable Lions
20:08 Cameroon yanusurika hapa. dakika mbili tu baada ya kipindi hichi cha pili kuanza.
20:08 Matokeo bado ni Mexico 0-0 Cameroon
20:07 Kipindi cha pili kinaanza hapa.
20:06 Mexico walitawala kipindi cha kwanza cha mechi hii ya kwanza inayohusisha timu kutoka Afrika
20:04 Refarii waendelea kuibua hisia kali kutokana mamuzi yao uwanjani.

0 comments:

Chapisha Maoni