Jumapili, Juni 15, 2014

BONGO MOVIE WAOMBEWA KUVUNJA ROHO YA UMAUTI

‘’MATESO basi, damu ya Yesu yatosha’’.  Hiyo ni kaulimbiu iliyotolewa katika Kanisa la Nchi ya Ahadi lililopo Sinza-Kamanyola jijini Dar, chini ya Mchungaji Kiongozi Harris Kapiga, wakati wa maombi maalumu kwa ajili ya wasanii wa Bongo Muvi ili kuvunja roho ya mauti juu ya tasnia hiyo ya filamu ambayo imewakumba wasanii wake. 
Maombi hayo pia yalikuwa ni kuwaombea ulinzi wote waliomo na wanaotamani kuingia katika tasnia hiyo.
Maombi hayo yaliwakilishwa na Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Saimon Mwakifwamba, wasanii na waimbaji Bahati Bukuku, Dotnata na wengineo.

0 comments:

Chapisha Maoni