Jumapili, Juni 15, 2014

WANAUME WANAONYANYASWA NA WAKE ZAO WATAKIWA KUTOA TAARIFA KWA MADAWATI YA JINSIA

SERIKALI imewataka wanaume kutoona haya na kufika kwenye madawati ya kijinsia yaliyopo katika vituo vya polisi nchini kutoa taarifa wanapofanyiwa vitendo vya kikatili na wake zao.
Kauli hiyo ilitolewa mjini hapa jana na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba, alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika.
Alisema kwa kipindi kirefu wanaume wamekuwa waoga kutoa taarifa pale wanapofanyiwa vitendo vya kikatili na kuishia kulalamika pembeni na kuwa wanyonge kwa kuona kuwa wanawake wanapendelewa kuliko wao.
Waziri Simba, aliongeza kuwa ni wakati wa jamii kuendelea kuwa wawazi na kutoa taarifa mara kwa mara wanapokutana na vitendo hivyo, hasa kwa watoto, ili viweze kufanyiwa kazi na kuchukuliwa hatua stahiki.

0 comments:

Chapisha Maoni