MSANII wa muziki na filamu Bongo, Snura Mushi amefunguka kwamba tuzo
saba za Kilimanjaro alizopata msanii mwenzake, Nasibu Abdul alistahili
kuzipata kwani anajituma.
Snura alisema Diamond ni mwanamuziki
anayejituma sana pia ni mbunifu na juhudi zake ndizo zimemfanya ashinde
tuzo zote hizo.
Mimi nilikuwa kwenye kipengele cha msanii chipukizi lakini haikuwa bahati yangu, naamini wakati wangu ukifika nitapata tuzo sina haraka ila kwa shemeji Diamond alistahili kupata
alisema Snura.





0 comments:
Chapisha Maoni