Mtangazaji wa Radio Times FM, Hadija Shaibu ‘Dida’ amezua
timbwili baada ya kung’ang’aniwa na mwanamke mwenzake aliyedaiwa kutaka
kumshawishi afanye naye mapenzi ya jinsi moja (usagaji).
Dida alikumbwa na ishu hiyo, Alhamisi ya wiki iliyopita ndani ya
Ukumbi wa Mango Garden, Kinondoni jijini Dar, wakati Kundi la Mashauzi
Classic, lilikuwa likiangusha burudani.
Katika tukio hilo
lililoshuhudiwa na chanzo chetu, mwanamke huyo aliyetajwa kwa jina
moja la Addy ambaye anadaiwa kukubuhu kwa tabia hiyo chafu ya usagaji.
Ilisemekana kwamba mwanadada huyo alianza kumzengea Dida kwa kumsemesha huku akimuonesha pozi za kimahaba.
Pamoja na Dida kumpuuza, Addy alifika mbali na kuanza
kumshtua kwa kutokea nyuma yake kwa kumtekenya huku akimkonyeza na
kumshawishi waongee vizuri.
Kutokana na vitendo hivyo, Dida alipandwa na hasira na kuchukua chupa kutaka kumpasua ndipo Addy naye akawa anahangaika kujitetea na kusababisha vurugu katika eneo hilo, shukrani ziwaendee wasamaria wema waliwatuliza.
Kutokana na vitendo hivyo, Dida alipandwa na hasira na kuchukua chupa kutaka kumpasua ndipo Addy naye akawa anahangaika kujitetea na kusababisha vurugu katika eneo hilo, shukrani ziwaendee wasamaria wema waliwatuliza.
Dida alisema:
Huyu dada ni muda mrefu alikuwa akinisumbua hapa ukumbini, mwanzo nilikuwa sijajua anachotaka kumbe ni mshenzi kabisa, anataka kunifanya vitendo vya kisagaji, amenikera sana.




0 comments:
Chapisha Maoni