Jumatatu, Mei 19, 2014

MAPYA YAIBUKA KIFO CHA ADAM KUAMBIANA...SUMU IMEHUSIKA...ALIKUWA NA MKE WA NDOA NA MTOTO AMBAO HAWAKUFAHAMIKA...ALIKUWA NA UHUSIAMO WA KIMAPENZI NA STARA THOMAS!!! BAJETI YA MAZISHI MILIONI 5

KIFO cha ghafla cha mwigizaji na mwongoza filamu za Kibongo, Adam Philip Kuambiana  kimeibua mazito ya kutosha, Uwazi limeshika kitu mkononi.
Moja kati ya mazito hayo ni kuwepo kwa madai kwamba marehemu alikula au alilishwa sumu kupitia chakula.
Kwa mujibu wa rafiki mmoja wa karibu wa Kuambiana aliyeomba hifadhi ya jina lake, marehemu Kuambiana asingekufa ghafla kama tatizo lilikuwa vidonda vya tumbo au kisukari, ila kuna sumu iliingia tumboni mwake kupitia chakula.
Siku ile Kuambiana alikuwa ana pesa, alianza kunywa pombe kuanzia asubuhi lakini pia alikuwa anakulakula kila alipojisikia. Naamini katika kulakula huko ndiko alikumbana na janga hilo
alisema rafiki huyo.
Mtu huyo wa karibu alikwenda mbele zaidi kwa kudai kwamba ana wasiwasi na baa moja ambayo hakuitaja kwa jina kwamba huenda marehemu alikula hapo kwani alikuwepo kwa muda mrefu siku ya Ijumaa.
Unajua ninaposema alikula chakula chenye sumu sina maana  wahudumu walimwekea sumu kwa makusudi. Ila siku hizi kuna ‘food poison’ (sumu kwenye chakula) ambayo mtu anaweza kujikuta anakula kupitia chakula, soda au juisi bila kujijua,
alisema mtu huyo.
Wakati rafiki wa karibu wa Kuambiana akiwa na wasiwasi na sumu, Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ ambaye alisema habari zilizoenea ambazo yeye amezisikia ni kuwa marehemu alikunywa dawa (hakusema dawa gani) pia akanywa bia jambo ambalo kama ni kweli alitengeneza sumu mwilini.
Binadamu wanasema mengi lakini mimi nilichosikia marehemu alikunywa dawa halafu akanywa bia zake na ndiyo chanzo cha kifo chake cha ghafla.
Lakini mimi ninachoamini yule bwana amekufa kwa sababu ya vidonda vya tumbo (ulcers). Lakini pia alikuwa akisumbuliwa na kisukari (diabetes).
Unajua alipewa masharti asinywe pombe halafu msosi uwe wa uhakika sasa inaonekana kwenye kuyazingatia hayo masharti ndiyo ikawa shida kidogo
alisema Steve Nyerere.
Nje ya Hospitali ya Mama Ngoma, Mwenge jijini Dar, Jumamosi iliyopita ambako wasanii walikusanyika kuuchukua mwili wa Kuambiana na kuupeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili gumzo lilikuwa ‘kumbe Kuambiana alikuwa na mke!’
Ni baada ya mwanamke mmoja aliyejulikana kwa jina la Janeth Rithe ambaye ni Diwani wa Kunduchi kwa tiketi ya Chadema  kufika akiwa analia. Ilibainika kuwa, mwanamke huyo ndiye mke wa ndoa wa Kuambiana na walizaa mtoto mmoja .
Kuibuka kwa Janeth kuliibua maswali kutoka kwa wasanii mbalimbali wakiwemo wadau wa filamu ambao pia walikuwepo. Wengi walijiuliza ilikuwaje marehemu alitangaza ndoa na mwanamuziki wa Bongo Fleva, Stara Thomas mwaka juzi wakati ana mke wa ndoa?
Wengi walisema huenda walitaka ‘kiki’ ya sanaa kwani licha ya kuanikwa kwa uhusiano wao pia Stara alikuwa akitangaza kutoa albamu yake ya Injili iliyojulikana kwa jina la Nani ni Mshamba?
Kufuatia gumzo la uhusiano huo, juzi Uwazi lilimtafuta Stara kwa njia ya simu ya mkononi na kumuuliza kuhusu hilo ambapo alisema:

Ni kweli tulikutana na Kuambiana na tulipanga kuoana. Lakini kuhusu mke yeye aliniambia alimpa talaka. Kwa hiyo alikuwa huru.
Hata hivyo, tulipeana muda wa kusomana tabia. Oktoba mwaka juzi (2012) tulitofautiana kidogo tukavunja uhusiano. Tukawa tuko pamoja kwa ajili ya sanaa tu, hasa filamu
alisema Stara.
Stara aliendelea kuweka wazi kwamba, Jumamosi ya kifo chake, Kuambiana alimpigia simu saa mbili asubuhi akamwambia anajisikia kuumwa sana.
Alisema anajisikia kuumwa sana, akakata simu hapohapo. Baadaye nikasikia anapelekwa hospitali, mara nikasikia amefariki dunia
alisema Stara.
Habari zaidi zinadai kuwa, marehemu alizaa na Janeth mtoto mwenye miaka 6 sasa aitwaye Miriam lakini ndugu wa marehemu wamedai mtoto huyo si wa Kuambiana huku ndugu wa mwanamke wakidai ni wa marehemu.
Marehemu Kuambiana anazikwa leo Jumanne kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar baada ya kuagwa kwenye Viwanja vya Leaders Club.
Marehemu anakwenda sambamba na marehemu Steven Kanumba kwa siku ya kufa (Jumamosi), kuagwa (Leaders Club) kuzikwa (Jumanne) na makaburi (Kinondoni).
Kwa mujibu wa Steve Nyerere, bajeti nzima ya msiba huo ni shilingi milioni tano na Bongo Movie imebeba jukumu la mazishi kwa asilimia 95 kuanzia jeneza, maji siku ya kuagwa Leaders na kaburi.

0 comments:

Chapisha Maoni