Jumatatu, Mei 19, 2014

ILE NDOA YA MILIONI 96 YA MBUNGE VICKY KAMATA IMEOTA MBAWA!!! KUNA ASILIMIA 90% ZA KUTOFUNGWA...SABABU IKO HAPA

ILE ndoa inayodaiwa ikifungwa harusi yake itatafuna shilingi milioni 96 kati ya Mbunge wa Viti Maalum Geita kwa tiketi ya CCM, Vicky Paschal Kamata na mwanaume aliyejulikana kwa jina la Charles iko katika hatihati ya kufungwa kutokana na kuibuka kwa mizengwe.

Habari za ndani zinadai kuwa mizengwe iliyoibuka katika hatua za mwisho zimemfanya mwanaume huyo kuamua kubatilisha ndoa ambayo ilikuwa ifungwe Mei 24, mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Kuna mizengwe mingi sana kwenye hii ndoa japokuwa iko katika hatua za mwisho lakini hatihati. Wapo watu wanasema kuwa mwanaume  anadaiwa ana mwanamke mwingine, wengine wanasema ana mchumba ameshamlipia mahari kwa wazazi wake kwa hiyo mambo yameshajulikana na jamaa akaona aachane na ndoa hiyo.
Lakini katika yote hayo, ukweli ni kwamba kuna asilimia tisini ya ndoa kutofungwa hiyo Mei 24 ndicho ninachokijua mimi
alisema mtu mmoja wa karibu na familia ya wachumba hao.
Vicky alipotafutwa kwa njia ya simu Jumamosi iliyopita iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa.

0 comments:

Chapisha Maoni