
Akizungumza na wandishi wa habari katibu mkuu
kiongozi Mh Ombeni Sefue amesema serikali imesikitishwa sana kuona
wapo baadhi ya watu wanaodhiriki kusema kuwa hati hiyo haipo .
Akasema pia kwamba ni kwa busara za
mwenyekiti wa bunge maalum l katiba akiona kuna haja ya hati hiyo
kupelekwa katika bunge maalum serikali ipo tayari.
Aidha akasema kuwa zipo hati ambazo
serikali inazihifadhi kwa umakini mkubwa ili kuhakisha kuwa
zinaendelea kubaki salama kwa kizazi cha sasa na kizazi kijacho.
Kiongozi huyo akaongezea kuwa ni matumaini ya
serikali kuwa baada ya kuitoa hati hiyo hadharani watu
wataendelea na mambo ya msingi yaliyopo mbele yao na siyo kuendeleza
malumbano ambayo hayana tija kwa taifa.
0 comments:
Chapisha Maoni