Jumanne, Aprili 15, 2014

RAY AKANA KUWA NA MPANGO WA KUMUOA CHUCHU HANS

Vincent Kigosi ‘Ray The Greatest’ amefunguka kuwa hana mpango wa kumuoa mwanadada Chuchu Hans kama inavyodaiwa na baadhi ya watu.

Akijibu swali aliloulizwa na wanahabari wetu hivi karibuni, kuhusiana na kudaiwa kuwa baada ya mpenzi wake huyo kupewa talaka ana mpango wa kufunga naye ndoa kama ilivyokuwa inadaiwa ambapo alikataa katakata suala la yeye kufunga ndoa na Chuchu.
 “Sina mpango wa kuoa ndugu yangu, hayo ni maneno ya watu ambayo yapo tu mitaani ila kwa sasa niko njiani naenda gym baadaye nitakutafuta tuongee.” alisema Ray.
Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa muigizaji huyo kufunguka kuhusiana na suala la ndoa na swali linakuja, je, Chuchu anafahamu kuwa anachezewa tu? Jibu analo mwenyewe moyoni mwake.

0 comments:

Chapisha Maoni