Rais Bashar al-Assad wa
Syria amesema kuwa, nchi yake itaushinda mgogoro wa sasa unaochochewa na
kuungwa mkono na madola ya kigeni na kwamba, nchi hiyo itazidi kuwa na
nguvu.
Rais Assad amesema hayo katika mazungumzo yake mjini Damascus na
ujumbe wa wataalamu wa Kiislamu na kusisitiza kuwa, hali ya sasa ya
Syria ni bora kuliko huko nyuma na kwamba, nchi hiyo itafanikiwa
kukivuka kwa ushindi kipindi hiki cha
Waziri Mkuu wa Syria
amezikosoa vikali nchi zinazowaunga mkono wanamgambo wanaopigana dhidi
ya serikali ya Damascus. Aidha Waziri Mkuu wa Syria amewapongeza
wananchi wa nchi hiyo kutokana na kusimama kwao kidete dhidi ya makundi
ya kigaidi na kusisitiza kwamba, mwaka huu utakuwa mwaka wa amani na
uthabiti kwa nchi hiyo ya Kiarabu.



0 comments:
Chapisha Maoni