Jumanne, Aprili 04, 2017

WEMA SEPETU KUSHINE KATIKA JARIDA LA KENYA 'TRUE LOVE'

Safari yake ilianza rasmi mwaka 2006 alipojitwalia taji la Miss Tanzania, akaendelea kujenga jina lake taratibu alipoingizwa rasmi katika ulimwengu wa filamu Tanzania na marehemu Steven Kanumba, akaendelea kukaa katika kilele cha ustaa kwa miaka 10 kutokana na kufanya mambo mengi yaliyovutia watanzania wengi kupitia kampuni yake ya Endless Fame, na hata kuingia katika siasa ndani ya CCM. 
Sasa anaendelea kukaa kwenye vichwa vya watu baada ya kuingia katika Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kama haitoshi hivi karibuni tutamuona katika jarida kubwa kutoka nchini Kenya la TRUE LOVE! Anaitwa Wema Abraham Sepetu.
Katika ukurasa maaumu wa instagram wa jarida hilo waliyaandika haya:
This month Tanzania’s Sweetheart, the gorgeous @wemasepetu graces our cover. She opens up about Money, Men, Love and Loss. Be sure to grab a copy to see what she has been up to and also read about Easter plans and gateways. Happy new month’- True Love Magazine East Africa

0 comments:

Chapisha Maoni