Jumanne, Aprili 04, 2017

WAFANYABIASHARA WATAWANYWA KWA SILAHA ZA MOTO MWENGE

Jeshi la Polisi limetumia silaha za moto kuwatawanya wafanyabiashara katika eneo la Mwenge, wilayani Kinondoni leo.
Taharuki iliwakumba wakazi wa eneo hilo mara baada ya polisi hao kuanza kuwatanya wafanyabiashara hao waliofunga barabara wakishinikiza magari yaruhusiwe kupaki katika eneo hilo.
Inaelezwa kuwa polisi wamezuia watu kupaki magari katika eneo hilo hali iliyosababisha wafanyabiashara hao kutofungua biashara zao leo. 
Akizungumza na gazeti hili, mmoja wa wafanyabiashara na shuhuda wa tukio hilo, Musa Godwin alisema polisi walifika sokoni hapo saa12 asubuhi na kutawanya wafanyabiashara waliofunga barabara kuzuia polisi magari yasiegeshwe eneo hilo.
"Walifika hapa sokoni saa 12 asubuhi na baadhi ya watu walifunga njia ikasababisha polisi wapige risasi hewani, hadi sasa wanazunguka hapa kuzuia magari ambao ni wanunuaji wetu," alisema Godwin. 

Mwananchi.

0 comments:

Chapisha Maoni