Jumanne, Aprili 04, 2017

BIASHARA KATI YA TANZANIA NA UGANDA YAPOROMOKA

Katibu mkuu wa wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki ya Tanzania Bw. Ramadhani Mwinyi amesema, thamani ya biashara kati ya Tanzania na Uganda imeshuka tangu mwaka jana.
Amesema, mwaka jana thamani ya biashara kati ya nchi hizo mbili ilifikia dola milioni 98 za kimarekani, na kwamba nchi hizo zinatakiwa kufanya juhudi kukabiliana na changamoto hiyo.
Pia amesema, sekta nyingi kutoka nchi hizo mbili zinatakiwa kutafuta chanzo cha kusababisha kushuka kwa biashara kati yao, hali isiyolingana na ushirikiano na uhusiano imara kati ya nchi hizo mbili.

0 comments:

Chapisha Maoni