Jumatatu, Aprili 03, 2017

TRUMP KUFIKISHWA MAHAKAMANI??

Jaji mmoja wa Mahakama ya Shirikisho ya jimbo la Kentucky la nchini Marekani amemtuhumu Rais Donald Trump wa nchi hiyo kuwa alichochea machafuko wakati wa kampeni za uchaguzi.
Hata hivyo kwa mujibu wa Press TV, David G. Hill, jaji wa mahakama moja ya shirikisho la Marekani huko Kentucky amesema kuwa, Donald Trump amekanusha madai yaliyotolewa dhidi yake ya kwamba alichochea machafuko wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2016.

Pamoja na hayo, jaji huyo ametoa hukumu inayoruhusu kufuatiliwa mashtaka yaliyofunguliwa dhidi ya Trump na timu yake ya kampeni. 
Jaji huyo wa Mahakama ya Shirikisho ya Marekani aidha amesema, kuna ushahidi wa kutosha wa kuthibitisha kwamba kulitokea machafuko wakati wa kampeni za uchaguzi za Donald Trump, na kusema kwamba rais huyo wa Marekani alisababisha machafuko hayo.
Mawakili wa Donald Trump wamefanya juhudi za kuzuia kesi za walalamikaji watatu ambao wanasema kuwa, mwezi Machi 2016 walishambuliwa kwa kupigwa na kutukanwa na wafuasi wa Trump wakati rais huyo wa Marekani alipokuwa anahutubia wafuasi wake katika jimbo la Kentucky. 
Wanawake wawili na mwanamme mmoja wamefungua kesi mahakamani dhidi ya Donald Trump wakilalamika kuwa, walishambuliwa na kutukanwa na wafuasi wa Trump kwa amri ya rais huyo wa Marekani.
Matamshi ya jaji huyo wa Mahakama ya Shirikisho ya Marekani ya kwamba Trump alichochea machafuko na kupigwa walalamikaji hao, linahesabiwa kuwa ni pigo jingine la kisheria kwa rais huyo mwenye chuki dhidi ya wageni, watu wasio Wazungu na pia dhidi ya Waislamu.

0 comments:

Chapisha Maoni