Alhamisi, Aprili 06, 2017

KIONGOZI WA FREEMASON AFRIKA MASHARIKI AFARIKI DUNIA

Aliyekuwa mfanyabiahsra maarufu wa Tanzania na kiongozi wa ‘Freemason’ Afrika Mashariki, Jayantilal Keshavji “Andy” Chande amefariki dunia leo Nairobi nchini Kenya.
Jayantilal Keshavji “Andy” Chande alizaliwa May 7, 1928 Mombasa Kenya, na wakati wa utoto wake aliishi Bukene mkoani Tabora ambako ndiko alikopata elimu yake ya msingi.
Elimu yake ya sekondari aliipata katika Shule ya St. Peter’s School iliyoko Panchgani, walaya ya Satara, Jimbo la Maharashtra nchini India. Baada ya kufanya vizuri katika mitihani yake ndipo alipopata jina jipya la ‘Andy’ ambalo ndilo alikuwa akilitumia mpaka mauti yalipomkuta.
Baada ya kumaliza masomo yake, alirudi nchini Tanzania na kuendelea kumsaidia baba yake katika shughuli za kibiashara.
Mnamo mwaka 1967 wakati azimio la Arusha lilipopitisha sera ya utaifishaji, mali nyingi zilitaifishwa na kuwa za serikali. Ujuzi aliokuwa nao Andy ulimfanya Mwl. Nyerere amteue kuwa Meneja Mkuu wa Shirika la Taifa la kuhifadhi nafaka (National Milling Corporation)
Mpaka kufikia mwaka 2015 alikwa na utajiri wa dola za kimarekani milioni 892 sawa na TZS trilioni 1.9.
Wakati wa uhai wake amewahi kupokea tuzo mbalimbali ikiwemo ya (Knight Commander of the Most Excellent Order of the British Empire) KBE mwaka 2003 ambayo ilikuwa ni kwa mara ya kwanza kupewa raia wa Tanzania.

0 comments:

Chapisha Maoni