Jumanne, Aprili 04, 2017

BAADA YA KITILA MKUMBO KUTEULIWA NA RAIS, ZITTO KABWE AMETOA MSIMAMO WAKE NA CHAMA

Zitto Kabwe, kiongozi wa ACT-Wazalendo amesema walifanya mashauriano kama chama ikiwemo Kitila Mkumbo, chama kimepokea uteuzi wa Kitila kuwa katibu mkuu. Uteuzi unaonyesha upinzani kuna watu wenye uwezo, weledi na uzalendo wa kuweza kutumika katika utumishi wa Umma.
Kitila ni mtumishi wa umma kwa sababu ni mhadhiri wa chuo kikuu cha Dar es Salaam kwa hio nafasi aliyopata ni kupanda cheo tu ndani ya utumishi wa umma, ni sawa kama angeteuliwa kuwa Vice Chancellor wa chuo kikuu.Kwa nafasi ya katibu mkuu, Ndugu Kitila hawezi kuendelea kuwa mshauri wa chama, nafasi ambayo inamfanya ahudhurie vikao vyote vya chama kuanzia ngazi ya chini mpaka kamati kuu na kamati ya uongozi.Prof. Kitila ameandika barua ya kujiuzulu ushauri wa chama, nimeipokea barua yake na nimemkubalia kujiuzulu kwake kuanzia Leo. Chama kinamshukuru sana mheshimiwa Kitila kwa wakati wote alichokitumikia chama toka tulipoanza chama hiki alipokuwa mshauri wa chama.Kaulimbiu yote siku zote ni taifa kwanza, leo na kesho hivyo tunamtakia kila laheri ndugu Kitila katika nafasi hii mpya, wizara ni kubwa na muhimu katika nchi yetu.Kwa hatua hii tumeona Rais ameamua kuunganisha nchi yetu kwa kufanya kazi na watu wote bila kuwabagua kwa itikadi zao za vyama. Watanzania ni wamoja na kauli za kuwagawa zinawaumiza zaidi. Tunaamini katika uteuzi huu, Rais ana nia njema na sisi tumempa baraka zote mwanachama wetu mwanzilishi wa chama kwenda kufanya kazi kwenye nafasi ya juu zaidi ya utumishi wa umma.
Alisema Zitto Kabwe

0 comments:

Chapisha Maoni