Jumanne, Machi 28, 2017

NDEGE YATEKETEA KWA MOTO IKIWA NA ABIRIA NDANI YAKE

Ndege moja ya shirika la ndege la Peru, Peruvian Airlines, iliyokuwa imewabeba wabiria 141, imeshika moto baada ya kutua kwa dharura katika uwanja wa ndege wa Jauja, katika milima ya Andes.
Shirika hilo la ndege limesema wote waliokuwa ndani wameokolewa salama na hakuna aliyepata majeraha.
Ndege hiyo iliteleza na kutoka nje ya njia inayotumiwa na ndege kupaa na kutua.
Wazima moto walifanikiwa kuuzima moto huo.
Uchunguzi umeanzishwa kuhusu kisa hicho.

0 comments:

Chapisha Maoni