Jumapili, Machi 26, 2017

NAY WA MITEGO KAKAMATWA NA POLISI MOROGORO ASUBUHI YA LEO, SABABU NI #WAPO?

Siku chache baada ya mwanamuziki Nay wa Mitego kutoa single yake mpya kwa jina la WAPO, wimbo ambao amesikika akipasuka uhalisia wa mambo yanayoendelea nchini, asubuhi ya leo taarifa kutoka mkoani Morogoro zinaeleza kuwa mbongo fleva huyo anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani humo pasipo sababu ya msingi kufahamika mara moja
Japokuwa inahisiwa kuwa kilichompelekea kushikiliwa ni suala la aina ya maneno aliyoyatumia katika wimbo wake, wapenzi na wadau wengi wa muziki wa bngo fleva wamehoji juu ya uhalali wa jeshi hilo kumshikilia Nay wakati wapo BASATA wenye mamlaka ya kufuatilia shughuli zote za wasanii Tanzania.(iwapo sababu ni wimbo #Bado)
Mwenyewe kupidia Instagram, Nay amethibitisha kukamatwa kwake:
Nimekamatwa kweli. Muda Huu nikiwa hotel Morogoro baada ya kumaliza Kazi yangu iliyo ni leta. Napelekwa Mvomelo Police.
Nawapenda Watanzania wote.
✊🏿✊🏿 #Truth
#Wapo

0 comments:

Chapisha Maoni