Jumamosi, Februari 27, 2016

NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI KUPIGA MARUFUKU MITUMBA

Viongozi wa nchi za Afrika Mashariki watakutana Arusha, Tanzania Jumatano ijayo kujadili upigaji marufuku uingizaji wa nguo zilizotumika au mitumba, magari yaliyotumika na bidhaa za ngozi kutoka nje ya eneo eneo hilo.
Taarifa iliyotolewa na jumuiya hiyo imesema itatafakari pendekezo la kuanzishwa viwanda vya utengenezaji magari na hivyo kupungua uingizaji magari yaliyotumika sambamba na kuimarisha viwanda vya nguo na ngozi katika nchi wanachama.
Kikao hicho cha Machi 2 pia kitajadili njia za kuanzisha Shirikisho la Kisiasa la Jumuiya ya Afrika Mashariki. Halikadhalika viongozi wa kanda hiyo watazindua paspoti za kielektroniki ambazo zitatumika kurahisisha usafiri kwa wananchi wa eneo hilo.
Watu wa Afrika Mashariki wamekuwa wakisubiri pasi hiyo kwa muda mrefu na hivyo kuzinduliwa kwake ni hatua muhimu katika kuimarisha ushirikiano wa nchi tano wanachama ambazo ni Burundi, Kenya, Rwanda, Tanzania na Uganda.
Katika kikao hicho, wakuu wa EAC watajadili ombi la Sudan Kusini na Somalia kutaka kujiunga na jumuiya hiyo.

0 comments:

Chapisha Maoni