Mwanamke mmoja,Dynel Lane,35,nchini Colorado amehukumiwa kifungo cha
miaka 120 baada ya kupatikana na hatia ya jaribio la mauaji na
mashambulizi ya kutumia kisu alipomdunga mwanamke mmoja mjamzito na
kukata kijusu kutoka kwa mfuko wake wa uzazi.
Michelle
Wilkins,27,ambaye alikuwa mwathirika alikuwa mjamzito wa miezi saba
mwezi Machi mwaka jana,wakati aliona tangazo mtandaoni linalohusika na
uuzaji wa vitu mbali mbali kwa kwenda nyumbani alikoishi Lane mjini
Longmont,ambapo alishambuliwa na Lane na kuwachwa katika hali mahututi.
Lane alichukua kijusu hicho katika hospitali jirani baada ya kufanya
mashambulizi hayo,akidai kuwa yeye alikuwa amepata ajali ya kuharibika
kwa mimba lakini polisi walifanya uchunguzi na baadaye kumtia mbaroni.
0 comments:
Chapisha Maoni