Ijumaa, Septemba 12, 2014

TANZANIA YAFANIKIWA KATIKA VITA DHIDI YA MADAWA YA KULEVYA

Mkuu wa kitengo cha kudhibiti dawa za kulevya nchini, Godfrey Nzowa amesema mawasiliano baina ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki yamefanikisha kudhibiti uingizwaji wa dawa za kulevya hapa nchini.
Akizungumza na Fichuo Tz, Nzowa ambaye pia ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) alisema wanafanyakazi kama timu kwa nchi za Afrika Mashariki na duniani kuhakikisha wanaweka mipango madhubuti ya kudhibiti uingizaji na uuzaji wa dawa hizo.
Akitoa mfano, alisema katika kipindi hiki ni vigumu kwa wauzaji kupata hata kilo moja hivyo wanalazimika kutafuta kwa gharama kubwa zaidi.

0 comments:

Chapisha Maoni