Ijumaa, Septemba 12, 2014

MSIKITI WA MTAMBANI WATEKETEA TENA KWA MOTO

MSIKITI wa Mtambani uliopo Kinondoni jijini Dar es Salaam, umeteketea tena kwa moto, huku bweni la wanafunzi wa kike pia likiathirika na moto huo ambao hata hivyo haukusababisha madhara yoyote kwa binadamu.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Camellius Wambura amethibitisha kutokea kwa tukio ambapo amedai kuwa chanzo cha moto huo bado haujafahamika.
Akizungumza katika eneo la tukio, Camellius Wambura alisema moto huo ulitokea majira ya saa 6 mchana na ulianzia kwenye chumba kimoja kinachotumiwa na wanafunzi wa kike wa kidato cha nne kwa ajili ya kujisomea.
Aliongeza kuwa chumba hicho hakikuwa na mtu wakati tukio hilo linatokea, huku akiweka wazi kuwa moto huo umeteketeza magodoro manne ambayo yalikuwa yakitumiwa na wanafunzi hao wa kike.
Alidai kuwa chanzo cha moto huo bado hakijafahamika, huku jeshi la polisi linaendelea kufanya uchunguzi ili kubaini chanzo cha moto huo.

0 comments:

Chapisha Maoni