Alhamisi, Septemba 04, 2014

KESI DHIDI YA BUNGE LA KATIBA YAANZA KUSIKILIZWA LEO

Mahakama Kuu nchini Tanzania leo imeanza kusikiliza kesi iliyofunguliwa na raia kupinga kuendelea kwa Bunge la Katiba linalokutana huko Dodoma. Kesi hiyo ambayo inasikilizwa na jopo la majaji watatu inasikilizwa katika wakati ambapo bado kunaendelea kushuhudiwa malumbano makali baina ya wabunge walioko bungeni na kundi la UKAWA ambalo limesusia bunge hilo kwa madai ya kupindishwa kwa baadhi ya vipengele vilivyowasiliwa kwenye rasimu ya katibu.

0 comments:

Chapisha Maoni