Jumanne, Julai 08, 2014

VERMAELEN HAJUI ATAKUWA WAPI MSIMU UJAO

Beki wa Arsenal 'The Gunners' Thomas Vermaelen amesema hajui atakipiga ndani ya timu ijayo kwa msimu ujao, huku kukiwa na taarifa mbalimbali kwamba anawaniwa na mashetani Manchester United.
Kwa sasa, yupo katika mwaka wa mwisho kabisa wa mkataba wake na anaweza kulamimika kuhama baada ya kuanza mechi kumi (10) tu msimu uliomalizika. 
Hivi karibuni, alijitokeza na kusema habari kuwa yupo mbioni kuamia United ni za uongo kwani yeye bado ni mchezaji halali wa Arsenal na akili yake kwa sasa imejidhatiti kuisaidia Ubelgiji huko Brazil. Lakini sasa, amejitokeza tena akisema hajielewi itakuwaje!
Kwa kweli sijui nitachezea timu ipi (msimu ujao), Iwe Arsenal au mahala pengine. Akili yangu yote ilikuwa kwenye kombe la Dunia, lakini nitajua nikishazungumza na Arsenal
Vermaelen, akiliambia gazeti la London Evening Standard.

0 comments:

Chapisha Maoni