Jumamosi, Julai 12, 2014

UTATA KATIKA HABARI YA MWANANCHI JUU YA KIFO CHA BALLALI

Kwanza, ukilisoma vizuri gazeti la Mwananchi toleo la jana 12/07/2014 kwenye ile habari inayohusiana na kifo cha David Ballali, gazeti linasema kuwa iliwachukua Siku tatu kulitafuta kaburi la marehemu Ballali.
Ilibidi wamuulize mtunza makaburi, ndiye aliyewaelekeza kaburi lilipo.
Wakati huo huo gazeti hili linadai kuwa Ballali alizikwa na ndugu zake wa karibu, ikiwa na maana kwamba, hao ndugu wa karibu walikuwa wanafahamu alipozikwa marehemu David Ballali.

Swali:-
Kulikuwa na ulazima gani wa mwandishi wa gazeti hili kumuuliza mtunza makaburi badala ya kuwauliza hao ndugu wa karibu na marehemu waliotajwa kuhusika kwenye shughuli za mazishi!
Anyway, sote tunatambua kwamba David Ballali alikuwa mtumishi wa umma nikiwa na maana kwamba, alikuwa Kiongozi mwandamizi wa Serikali tena Kiongozi wa nafasi ya juu na nyeti sana (Gavana wa Fedha), hivyo basi, ilikuwaje Serikali ikashindwa kumtuma mwakilishi toka Serikalini, ambaye angeungana na wanandugu hao katika shughuli za mazishi ya marehemu huko nje ya Nchi!
Nimeuliza jambo hili kwa sababu hakuna mahali ambapo mwandishi ametaja aidha Jina au Cheo cha mtumishi wa Serikali aliyeongozana na wanandugu wa marehemu Ballali kwenda kuhudhuria mazishi yake.
Utata bado ni mwingi sana katika habari ile ya mwandishi kuhusu kifo cha Ballali.
Pili, ukiitazama vizuri hiyo Picha iliyotolewa na gazeti hili ikilionyesha kaburi la marehemu Ballali, utaona wazi kabisa kuwa eneo hilo ni kaburi la marehemu Ballali pekee ndilo linaloonekana.
Swali:-
Kwa nini mwandishi huyu anayetuaminisha kwamba alifika eneo la kaburi, hakupiga Picha kubwa ambayo pia ingeyaonyesha makaburi mengine, kwa sababu tayari walikuwa eneo la makaburini, au hakuna Picha yoyote ya ukumbusho aliyochukua akiwa pamoja na wenyeji wake aliofika nao katika eneo hilo la makaburi, bila kumsahau mtunza makaburi aliyemwelekeza mahali kaburi lilipokuwa!
Haya ni maswali magumu sana ambayo ninaamini mwandishi huyu akiyaona, hatatamani ku-like au ku-comment kwenye post hii, bali atapita kwa speed ya ajabu.
Tatu, bila shaka ndugu wa marehemu ambao gazeti hili linadai ndio pekee waliohudhuria mazishi ya Ballali, watakuwa walirekodi tukio lote.
Swali:-
Kwa nini mwandishi wa gazeti hili hakuhangaika kuwatafuta hao ndugu wa marehemu Ballali waliohudhuria mazishi hayo ili wampe briefing ama more information kuhusiana na namna ambavyo mazishi yalifanyika!
Nne, mwandishi anadai kuwa pasipo na shaka, hilo ni kaburi la Ballali kwa mtizamo wa nje.
Swali:-
Mwandishi huyu anao uhakika au udhibitisho gani tofauti na huo muonekano wa nje wa kaburi la marehemu kwamba aliyezikwa pale ni yeye Ballali kweli!
Kwa sababu kitendo cha kulitazama tu kaburi kwa muonekano wa nje, hakiwezi kuwa na mashiko ya kufikia hatua ya kuuaminisha umma wa watanzania wenye nia na shauku kubwa ya kuujua undani wa utata wa kifo cha David Ballali kwamba kaburi hilo ni la kwake, kwa hili hata mtu mwenye uwezo mdogo wa kuchanganua mambo, ni lazima atapingana na wewe, manaake ni hoja dhaifu sana.
Kuna Critical thinkers, Great thinkers na wapo Poor thinkers, hivyo unapotoa habari kama hizi ambazo ni very sensitive kwa umma, utarajie kukihadaa kikundi kidogo sana cha watu.
Mhe.Msigwa aliwahi kusema, "Huu ni mfumo wa akili ndogo kujaribu kuitawala akili kubwa".

0 comments:

Chapisha Maoni