Jumapili, Julai 13, 2014

TUZO MBALI MBALI KATIKA WORLD CUP 2014

Zifuatazo ni tuzo mbalimbali zilizogawiwa kwa wachezaji mahili katika fainali za Kombe la Dunia nchini Brazil mwaka huu.
adidas GOLDEN BALL
Hii ni tuzo ya mpira wa dhahabu ambayo hupewa mchezaji aliyefanya vyema kwa ujumla katika mashindano, mshindi ni LIONEL MESSI wa Argentina.
adidas GOLDEN BOOT
Hii tuzo buenda kwa mchezaji aliyefunga goli nyingi katika mashindano, amechuchuka JAMES RODRIGUEZ wa Colombia, ambaye ametia tia nyavu mara sita (6) katika michuano hii.
adidas GOLDEN GLOVE
Hii tuzo hupewa golinyanda bora kabisa kutoka michuanoni, ameichukua MANUEL NEUER kutoka Ujerumani kutokana na udakaji bora kabisa kipindi chote cha michuano.
Hyundai YOUNG PLAYER AWARD
Hii ni ya mchezaji mwenye umri mdogo na aliyefanya vyema kabisa katika michuano. Amechukua kiungo PAUL POGBA kutoka France kutokana na uchezaji mahiri kabisa dimbani.
FIFA FAIR PLAY AWARD
Tuzo hii hupewa timu ambayo imeonyesha kiwango cha juu kabisa cha nidhamu katika michuano, hata hivyo, moja ya vigezo vikubwa ni kwamba lazima timu hiyo iwe imevuka mzunguko wa kwanza na kuingia katika hatua ya mtoano ndipo itafikiriwa kuwania tuzo hiyo. TEAM COLOMBIA, ndio wametwaa tuzo hii ikiwa imeonyesha nidhamu thabiti safari hii, mara ya mwisho ilikuwa Spain mwaka 2010.

0 comments:

Chapisha Maoni